HADITHI YA BABA MASUMBUKO SEHEMU YA KUMI NA MOJA(11)


                                                               HADITHI YA
                                                               BABA MASUMBUKO



Mwandishi:PAUL M,YAHILIMA
Facebook:Yahilima PM
                                                               SEHEMU YA KUMI NA MOJA

Nilipoanza kunyata ili nikatekeleze unyama nikaona si sawa nikimuua kwa njia rahisi maana niliogopa majirani kama watasikia kelele,wazo lililonijia ambalo lilikuwa sahihi ni kwenda kwenye nyumba ya jirani maana pale kulikuwepo na nyumba iliyoezekwa nyasi ambayo huwa wanaitumia kama jiko na kulazia mifugo yao uamzi niliokuwa nao ni kwenda kuichoma ile nyumba ili hata kama nikiwa natekeleza mauaji kelele za kilio kisisikike,nilienda hadi kwa jirani kutokana na ile nyumba kuwa karibu na shamba,nilienda taratibu nikawasha njiti tatu za kibiriti kwa mkupuo nikazirusha juu ya ile nyumba  bila kuchelewa nikakimbia kwa kasi kuja kummaliza mke wangu kadri nilivyozidi kuisogelea nyumba ya mke wangu mkubwa kelele za kuomba msaada zilisikika kwenye nyumba niliyoichoma moto na ndani ya muda mfupi uliopita,kila upande wa kijiji yowe zilisikika kama kawaida wanakijiji walizidi kusogea ili kutoa msaada kwenye ile nyumba ya jirani niliyoichoma,

Nilipoona kuwa wananchi wameweka umakini kwenye tukio la kuungua kwa nyumba kwa upande wangu niliona kuwa ile ilikuwa ni nafasi ya mimi kutekeleza  unyama nilioupanga,nikaanza  kutembea kwa kunyata hadi mlangoni kwenye nyumba ya mke wangu mkubwa,kwa msaada wa mwanga wa taa ya koroboi nilimwona mke wangu akiwa sebuleni muda huo alikuwa anaendelea kula taratibu,nilijawa na hasira sana hasa nilipokumbuka mambo aliyonitendea,nilirudi nyuma kama hatua tatu hivi usawa wa mlango,nikavuta kasi nikahesabu mara tatu nikauparamia ule mlango na kwa bahati nzuri komeo ilikatika na mlango ukafunguka na kabla mke wangu hajasimama niliingia kwa kasi na bila hata kufikilia niliinua panga  nililokuwa  nalo nikalishusha kwa nguvu kwa bahati nzuri lilitua katikati  ya kichwa chake na kukitenganisha kama vile chungwa linapokatwa nikamkagua kama alikuwa amefariki tayari nikajilizisha kuwa tayari alikuwa amesha kufa,nikatoka taratbu kwenye ile nyumba kwa bahati nzuri hakuna mtu aliyekuwa ananiona.
Baada ya mauaji yale nikatokomea kuelekea kwenye mto wa karibu ili nikaoge na nikajisafishe,nilifika mtoni nikaoga na nikalisafisha nilipohakikisha kuwa  usafi umekamilika nikavaa nguo zangu vizuri na kuanza safari ya kuelekea sehemu ambayo mganga aliniambia tukutane baada ya kukamilisha lile zoezi nilitembea kwa haraka na baada ya muda mfupi nilifika sehemu husika.

Sasa masanja umekuwa masanja yaani umekuwa mweupe kabisa itabidi uniletee ng`ombe watatu ili uwe kamili kabisa

Sasa mganga nilete ng`ombe wa nini we nipe dawa kama tulivyoelewana,mbona unabadilisha maelezo

Najua hujui na mashariti ya uganga huyajui vizuri unakichwa kigumu

Muda ule naendelea kuongea na Yule mganga kadiri muda ulivyozidi kusogea mbele chuki juu ya Yule mganga ilizidi hadi nikashindwa kujizuia hadi machozi yakawa yananitoka mfululizo sikujua kwa nini,muda huo mimi nilikuwa nimesimama wima na mwili ulikuwa umekakamaa sana na jasho lilizidi kunitoka sana,mganga alikuwa amekaa ila macho yake yalikuwa yakinitazama na nilivyomtazama kwa makini nikamwona akiwa na hofu sana sikujua kwanini anahofu hivyo na pale nilipomtazama sana hasira zilinijaa nikarusha ngumi kutoka kwenye mkono wangu wa kulia kutokana na uzito wa ngumi ile mganga alianguka chini,bila hata kuuliza chochote  mganga akaanza kujitetea na hapo ndipo nikaona ni njia nzuri ya kumdadisi,nikachomoa lile panga nililolitumia kumuulia mke wangu,nikakumbuka mambo yote mabaya aliyonitendea Yule mganga ikiwemo kutaka kuniua kule mlimani akiwa na watu wake,nikakumbuka mtego alionifanyia hadi nikaenda gamboshi,sikutaka kwendelea kufikilia nikalishusha panga kwa nguvu alipokuwa ameinama pale chini kwa bahati nzuri alifanikiwa kulikwepa na nilipomwangalia usoni roho ya huruma iliniingia,nikamshika kwa nguvu nikamkalisha kwenye jiwe lililokuwa kando,mganga aliniangalia kwa muda kidogo ila hasira nilizokuwa nazo mwanzoni zikanijia tena,nikampiga kofi zito la usoni kisha mganga akaanza kueleza jambo jipya kabisa ambalo lilinichanganya zaidi na hilo ndiyo linalofanya nikusimulie kisa hiki

Sema haraka,nitakukata mapingili pingili

Mke wako mdogo

Mke wangu mdogo kafanya nini?

Mke wako mdogo kabla hujamuoa alikuja nyumbani kwangu akiwa na shida,na shida yenyewe alikuwa anatafuta dawa ili apate mwanaume wa kumuoa,nilimpa masharti kabla ya kumpa dawa ilibidi atafute mtu aliyeolewa ambayo bado hajazaa kisha achote mchanga kwenye nyayo za miguu za huyo mtu,alilifanikisha zoezi hilo kwa muda mfupi na kwa bahati mbaya alichotza mchanga kwenye nyayo alimopita mke wako mkubwa masalu,alileta ule mchanga nikauwekea dawa ambayo ilikufanya wewe uanze kumchukia mkeo mkubwa tofauti na hilo pia tulimfunga mkeo mkubwa uzazi ili asiweze kuzaa na kweli alishindwa kupata ujauzito hali ambayo wewe ilikuchanganya akili hadi ukaamua kutafuta mke mwingine na kwa kuwa lengo langu na mkeo mdogo kabla ya kumuoa lilikuwa kutafuta mwanaume atakayemuoa mkeo mdogo,tulikufanyia dawa kisha wewe ukawa huoni  wanawake wengine zaidi ya mkeo mdogo ambaye kweli baada ya muda ulimuaoa, jambo ambalo ulikuwa unalitaka ambao ni kupata watoto ulifanikiwa kupata watoto wa kike,kutokana na mashariti ya dawa na mizimu mkeo mdogo hakutakiwa kuzaa mtoto wa kiume na ndiyo maana watoto wote kutoka kwa mkeo mdogo ni wakike wote na ukikumbuka siku ambayo mkeo mdogo alizaa mtoto wa kiume mbele yangu,mimi na huyo mkeo tuimuua Yule mtoto kisha wewe tulikulewesha kwa dawa na hukujua lolote lililoendela hadi tulipomaliza mipango yetu na wewe ulipata fahamu ulikuta mwanao tayari ameshakufa.naomba ujue kuwa hata wale watoto wa kike siyo wako ila wale watoto ni wangu mimi mganga na mkeo mdogo tulikuwa tunakutana mara kwa mara na kushiliki tendo la ndoa ila wewe hukujua hilo pia ulikosea kuuza ng`ombe zile tatu ili umpeleke shule masumbuko jambo hili ndiyo liliibua hasira tukaanza kuishambulia familia yako tena kwa sababu ile mali siyo yako bali ni yangu na mkeo mdogo, na tulikufanyia dawa mbegu zako za kiume zikawa hazina nguvu kabisa hili lilifanywa na mkeo mdogo uliyemwamini sana,alikunyoa nywele zako za sehemu za sili na akachukua mbegu zako akaleta tukachanganya kwenye dawa.uwezo wa Mungu ni mkubwa alikusaidia wewe na mkeo mkubwa mkampata mtoto mliyemuita Masumbuko,kitendo cha nyinyi kupata mtoto wa kiume kilitukera sana na tukaifanya umchukie mkeo mkubwa zaidi ya awali maana tulitumia kivuli cha sura yake ili aonekane mchawi,wewe kwa macho yako ya kawaida ulimuona mkeo kwenye sehemu mbalimbali na alionyesha dalili zote za uchawi lakini yule hakuwa yeye bali ni mimi na mkeo mdogo tulijificha kwenye kivui cha sura yake ili umchukie hadi umemuua leo kwa mkono wako ila kusema ukweli mkeo mkubwa uliyemuua hajui dawa wala haujui uchawi ila mkeo mdogo ndiye mchawi,na tambua kuwa mwanao masumbuko tumemtoa kafara gamboshi ili tupate madaraka

Baada ya maelezo hayo marefu yaliyouchoma moyo wangu kwenye kila neno,mganga aliomba nimsamehe akiwa bado anaendelea kunisihi nimsamehe,niliinyosha mikono yangu alipokuwa amekaa nayeye akaileta kwangu ila kabla haijanifikia nilichomoa panga nikalivulumisha kwa nguvu vidole vyote kumi vya mikono niliviona chini pale,muda huo sikuwa na huruma niliushika ule upanga kwa mikono miwili na kwa nguvu zangu zote nilimkata Yule mganga kwenye mapingiili matatu kisha lile panga nikalisimika pembeni ya mwili wa mganga na hiyo ndiyo sababu ya mimi kukimbilia Dar hadi leo naokota makopo sina mbele wala nyuma popote utakaponiona usiniite Masanja kifulambute ila niiteBaba Masumbuko na cha zaidi nakusihi usiamini waganga wa kienyeji wengi ni waongo muamini MUNGU tu.
                                         *******************MWISHO*********************
PAUL M,YAHILIMA
0788624797
0765084515
yahilimap@gmail.com

Comments

Popular posts from this blog

HADITHI YA BABA MASUMBUKO SEHEMU YA KWANZA (1)

HADITHI YA BABA MASUMBUKO SEHEMU YA NNE(4)

HADITHI YA BABA MASUMBUKO SEHEMU YA TATU(3)