HADITHI YA BABA MASUMBUKO SEHEMU YA KWANZA (1)
HADITHI YA
BABA MASUMBUKO
Mtunzi: PAUL M,YAHILIMA
0788624797
0765084515
Facebook yahilima pm
Tembelea http://mla-ukoko.blogspot.com
Mtunzi: PAUL M,YAHILIMA
0788624797
0765084515
Facebook yahilima pm
Tembelea http://mla-ukoko.blogspot.com
SEHEMU YA KWANZA
Wewe! huyu mwanamke asiyezaa bado hajaleta chakula hadi sasa?,
nilimuuliza mke wangu
mdogo naye akanijibu kuwamke mkubwa hajaleta chakula chochote kisha nikamwagiza
mke wangu mdogo afuate chakula maana ilikuwa ni kawaida yangu kula chakula cha
wake zangu wote na
hata kama nikitoka wiki moja lazima nikute mboga walizokula kwa siku ambazo
sikuwepo,baada ya muda mfupi mke wangu mdogo alirudi na nilipomuuliza kwanini hajaja na chakula
hakunijibu chochote moja kwa moja nikajua atakuwa amejibizana vibaya na mwenzake,nilikura kwa haraka na baada
ya kula nilimwita mke wangu mdogo naye akaja karibu na mimi,
nambie mume wangu nikupendaye kwa dhati ila mwenzako
mwanamke wako hanipendi yaani leo kanitukana
mwache tu dawa yake ipo jikoni na lazima atang`oka tu
mwache tu dawa yake ipo jikoni na lazima atang`oka tu
Halafu mume wangu hii mimba nahisi atakuwa mtoto wa kiume,
nataka nikufurahishe sana maana nimekuzalia watoto wawili wa kike sasa
unahitaji kidume
Nilitamani nimweleze mke wangu mdogo nilichopanga kumweleza
siku ile ila baada ya maelezo yake kuhusu mimba nilishindwa hata kumwambia na
siku ile nilipanga kumweleza kuwa nataka kwenda kulala kwa mke mkubwa kwa siku
ile kwa maana siku nyingi zilipita bila kulala kwa mke mkubwa,mke mdogo alienda
kutandika kitanda akaniacha sebuleni, ghafla nje mbwa walianza kubweka kama
kawaida ya maisha ya kijijini ilinibidi nitoke nje kwenda kuangalia kipi mbwa
wangu kinawafanya wabweke,ulikuwa ni usiku wenye giza sana uliotawaliwa na sauti za vyura zilizokuwa
zinasikika kutoka kwenye mto unaotenganisha kijiji chetu cha matongo na kijij cha
jirani cha sapiwi mkoani simiyu,kwa
mbali maji yalisikika yakipigana vikumbo kwenye mto kutokana na mvua iliyonyesha
jioni ya siku ile,nikiwa bado naangalia usalama pale nyumbani nilisogea kwenye
zizi la ng`ombe ambao jioni ile ndiyo nilitoka kuwachunga, ghafula mbwa waliokuwa
karibu na na mimi walikimbia kuelekea upande wa pili wa zizi na mimi nikajaribu kuelekea kule mbwa walipoelekea lakini kabla hata sijasogea
zaidi wale mbwa walirudi kwa kasi na kunipita nilipokuwa,sikuwa na lakufanya na
kwa sababu sikuwa hata na tochi yakunisaidia kuona kipi kimewafanya mbwa wangu
warudi tena kwa kasi hivyo,nilijawa na uoga nikakimbia nikaupalamia mlango
dhaifu wa nyumba ya mke wangu mkubwa, nilipofika sebuleni kutokana na utelezi
pale sebuleni nikaanguka ,mke wangu alipiga sauti yakuomba msaada kwa maana
alijua kavamiwa lakini nilimweleza kuwa ni mimi kwa haraka akaja nilipokuwa
nimeanguka.
Mume wangu pole kwa kuanguka jamani, tatizo gani limekupata?
Pumbafu wewe yaani umetega maji ili nianguke si ndiyo
?
Hapana sijakutega mume wangu si leo mvua imenyesha na nyumba
imevuja sana.
Sasa ulishindwa kuyatoa?
Samahani mume wangu nisame……..
Mke wangu hakumalizia maelezo yake nikampiga kofi la usoni
kwa haraka akarudi chumbani akaniacha pale sebuleni,aliendelea kulia kwa
machungu ila sikujali nikamwamuru awashe taa ya koroboi lakini hakuwasha jambo
hilo liliniudhi sana nikajawa na ghadhabu kama mbogo aliyejeruhiwa,nikatoka
sebuleni kwa lengo la kwenda kumwongezea kipigo nilipofika chumbani nikapapasa
kwenye ndoo ndogo aliyokuwa anatumia kama meza,nikapata kibiriti nikawasha
njiti kabla hata sijawasha taa nikamwona mke wangu akitokwa na damu nyingi sana
puani na mdomoni jambo hilo lilinitia hofu sana hadi njiti ile ikazimika na
nilipowasha njiti ya pili ili niwashe taa aina ya koroboi kwa bahati mbaya
haikuwa na mafuta,kutokana na hofu kubwa juu ya damu zinazoendelea kumtoka mke
wangu na kilio alichoendelea kukitoa niliamua kuichukua koroboi na kutoka
kwenye nyumba ile ili nifuate mafuta kwa mke wangu mdogo,nilitoka nje nikiwa
nakimbia bila kujua kumbe alikuwepo mbwa akiwa amejilaza mlangoni nikamparamia
nikaanguka na kiatu kimoja cha kata mbuga kikachomoka mguuni lakini sikujali juu
ya hilo nikaamka nikakimbia kwa haraka hadi kwenye nyumba ya mke wangu mdogo,
Wewe mwanamke fungua dirisha haraka?
Inakuwaje unagonga hodi dirishani na ulikuwa wapi muda wote
huo au ndo ulikuwa na limwanamke lako lisilozaa?
Acha maneno yako nipe mafuta haraka.
Niliamua kuwa mkali ndipo mke wangu mdogo alipoamua kufungua
dirisha na kuniwekea mafuta kwenye ile koroboi kisha nikaondoka kwa
haraka,nikafika chumbani kwa mke wangu mkubwa nikawasha taa,damu nyingi ilikuwa
imemwagika sana mle chumbani,nikatafakari kidogo nikaamua kwenda sebuleni kuchukua
maji ya mvua kwenye jagi nikarudi nayo chumbani nikamwagia mke wangu kichwani,damu
iliyokuwa inamtoka ikapungua taratibu hadi ikaacha kutoka kabisa kisha
nikasafisha mle chumbani kisha nikajitupa kitandani ambapo mke wangu alikuwa tayari amelala.
.
Mume wangu siku hizi
hunipendi,yani tokea umuoe mke mdogo wala hunijali na kumbuka ulimuoa kwa mali
tulizotafuta mimi na wewe na badaye umemjengea nyumba nzuri umeezeka mabati
kwake umemjengea tena slop kabisa halafu mimi bado niko kwenye nyumba ya nyasi
inayovuja kiasi hiki,tazama leo umeteleza na umenipiga mwenzako
.
Nitakujengea na wewe usijali.
Toa uongo wako hapa, kila siku unandanganya tu haya
wajengeewenye kuzaa.
Mke wangu aliongea mengi sana huku akiwa analia hadi
nikapitiwa na usingizi kutokana na uchovu wa siku ile,nikiwa bado usingizini
nilishituliwa na kitu kizito kilichotua kichani mwangu nilipofungua macho
nikakuta mke wangu akiwa ameshikilia rungu
Umenipiga rungu eti? sasa utanijua kuwa mimi ndo masanja
halisi
Nimekukomesha na wewe leo maana umezoea kunipiga tena toka kwangu kalale kwa
mkeo unayempenda ambaye huwa anakuzalia watoto tena niache peke yangu na
ukinisogelea nitakupa nundu nyingine kama hiyo haijakutosha ili uwe na mapembe
kabisa.
Mke wangu mkubwa aliongea kwa hasira nikaamua kutoka
chumbani kwake,nikatoka nje kwa hasira jambo la kwanza kulifikilia ni kwenda kwa mke wangu mdogo lakini nikaona ni
vigumu kumshawishi ili aweze kunifungulia usiku ule.Nikajipapasa kichwani
nikajikuta nina nundu kubwa iliyotokana na kupigwa kwa rungu na mke wangu
mkubwa,hali hii ilinipa uchungu sana na siku zote tokea nikiwa mdogo sikuwahi
kukubali kushindwa na mwanamke,nikaamua kurudi kulipiza kisasi nikaingia
taratibu mle chumbani kwa bahati nzuri nikamkuta mke wangu akiwa amesinzia
nikalitoa rungu karibu yake ambalo hasa ndilo lililokuwa linampa kiburi kisha
nikamwamsha na alipoamka tu nikampiga ngumi tumboni,ila kwenye mvurugano mle ndani
alibahatisha nafasi akaning`ata mkononi kitendo kile kilioniongezea hasira mara
mbili nikamrukia mke wangu nikamkaba
kooni kutokana na kumzidi nguvu hakuwa na uwezo wa kupambana na mimi tena baada
ya muda kidogo alipoteza fahamu…………………INAENDELEA
usipitwe na mwendelezo wa hii hadithi like blog kwenye link hiyo chini kisha share http://mla-ukoko.blogspot.com
usipitwe
usipitwe na mwendelezo wa hii hadithi like blog kwenye link hiyo chini kisha share http://mla-ukoko.blogspot.com
usipitwe
Comments
Post a Comment