HADITHI YA BABA MASUMBUKO SEHEMU YA TISA (9)



                                                                     HADITHI YA 
                                                                     BABA MASUMBUKO
Mwaandishi:PAUL M,YAHILIMA
Facebook:Yahilima PM
                                                                     SEHEMU YA TISA 

Baada ya kusikia ile amri ikiamuru nikamatwe na nikiwa msumbufu niuliwe niliogopa sana ila sikukata tama na dhamira yangu ya kutoroka ilikuwa palepale nikaanza kuteremka kutoka juu ya mlima kwa kasi sana lakini nilipobakiza eneo dogo tu ili nifike chini kabisa ya ule mlima na matumaini ya kutorka yakiwa yamenijaa nikasimama kwa sekunde kadhaa nyuma kama kuna anayenifuatilia lakini nikabaini kuwa hakukuwepo mtu anayenifukuza lakini nilipotazama mbele nilipokuwa naenda ambako ndiyo chini kabisa ya mlima nikaona kundi la watu likiwa linakuja  kwa kasi na baadhi walikuwa wameanza kupanda ule mlima huku wamewasha mwenge na kwa wakati huu wale watu wenye mwenge walikuwa wengi zaidi na walikuwa wanaimba lakini walipofika kwenye mlima  wakawa kimya na ule moto waliokuwa nao wakauzima kisha giza totoro liliufunika mlima wote,jambo la kushukuru mkononi nilikuwa na tochi lakini sikuweza hata kuiwasha nikaamua  kurudi kwa haraka juu kabla sijafika eneo la juu kabisa kwenye kilele cha ule mlima ambapo ndipo mganga nilimwacha nikazunguka kwa haraka nyuma ya  mlima ambako  kulikuwepo shimo ambalo nilikuwa nimeshaliona siku za nyuma nikatembea kwa makini ili sauti ya nyayo zangu asisikie mtu na kwa bahati nzuri nikafanikiwa kufika kwenye lile pango sikujali kama wameniona au la nikaingia kwenye lile shimo na sikujali nitakutana na hatari gani kwenye lile shimo refu bila kupoteza muda nikazama kwenye lile shimo nikawasha tochi nikaangalia kwenye kila sehemu kama kuna hatari yoyote lakini sikuona hatari zaidi ya popo wengi tu,nikiwa bado natafakari niliona mwanga kwa nje na mlima wote ukawa unaonekana hali hiyo ilinifanya nijue  kuwa wale watu wameshapanda kwenye mlima na wameshauzunguka wote,hata baada ya mwanga kuonekana kwenye ule mlima hakuna mtu aliyeweza kusikika akiwa anaongea chochote,ila baada ya dakika chache nje ya shimo nililojificha niliona kivuli cha mtu anapita lakini sikujua ni nani nilijawa na hofu kubwa nikajua nilipokuwa ninaingia kwenye shimo labda walikuwa wameniona na kutokana na hofu mkojo ukanitoka bila hata ya kujua na mwili wote ulikuwa umelowana kwa jasho,muda huo niliona kabisa siku yangu ya kufa itakuwa imefika japo tokea nizaliwe sijawahi kuingia kanisani hata tu kukanyaga mlangoni wala msikiti sikuwahi kuingia lakini nilimuomba sana Mungu aniepushe na watu wale wabaya.

Mimi ndo mganga ganungo ga walwa ishiishi lya boshishi mabogota gaza.

Ndiyo mkuu!

Nilipowaambia mkamateni mlifanya uzembe sasa yuko wapi? Narudia fanyeni juu chini mumkamate

Ndiyo mkuu!

Aje mzima au amekufa sawa?

Sawa mkuu!

Sauti iliyosikika nilikuwa naijua vyema,alikuwa ni mganga wa kienyeji na baada tu ya kutoa ile amri watu waliokuwa kwenye eneo lile wakasikia wanatawanyika na ila sauti ya mganga ikaendelea kusikika pale pale na nikasikia anaomba mizimu yake ili imuonyeshe nilipo,nikiwa bado nayasikiliza maneno ya mganga wazo likanijia kwa haraka wazo la kuingia zaidi kwenye lile shimo  moja kwa moja safari nisiyoijua mwisho wake huku nikimwomba Mungu kila hatua ninayopiga ili iwe ya kheri kusitokee mnyama au mdudu  wa kunidhuru,kulikuwepo na shimo refu na upana wake ulitosha kabisa kupita ila kwa mwendo wa kuinama,muda wote tochi niliyokuwa nayo nikamulika mbele nilipokuwa naelekea na kwenye mkono wa kushoto nikabeba mawe ya tahadhari ili chochote kitakachojitokeza niweze kupambana nacho na kadiri muda ulivyozidi kwenda hofu ilizidi kunijaa nikaanza kusali dua yangu ya mwisho na nikamuomba sana Mungu anisamehe makosa yangu yote,baada ya mwendo kama wa saa moja nikachoka sana kutokana na mwendo wa kuinama ikanibidi niangalie sehemu yenye usalama wa kutosha ili nipumzike baada ya kuhakikisha kuwa eneo lile ni salama nikakaa kwenye jiwe moja nikakaa,muda wote sikutaka kabisa niruhuusu usingizi unipitie lakini cha ajabu usingizi ukanipitia nikasinzia kilichonishitua ni maumivu makali niliyoyapata kwenye kidole kikubwa cha mguu wa kulia,maumivu yale yakanifanya nifumbue macho kwa haraka nikamwona ng`e akiwa anatokomea kwenye jiwe la jirani na nilipoweka mguu moja kwa moja nikajua aliyenigata ni ng`e na haikuwa mara ya kwanza kung`atwa na ng`e,nikalifunua lile jiwe alimokimbilia Yule ng`e kwa bahati nzuri nikamkuta nikachukua jiwe dogo nikampiga hadi akafa kisha nikaukata mkia wake ambao ndiyo huwa anatumia kung`atia na ndiyo wenye sumu kisha nikautafuna nikameza kidogo na mabaki yake nikabandika kwenye sehemu niliyong`atwa,baada ya muda kama nusu saa maumivu yakaisha,sikutaka kupoteza muda nikaanza safari tena sikuchukua muda sana nikiwa kwenye lile shimo kwa mbali nikaona mwanga nikazidi kupata hofu sana juu ya nini kipo kwenye ule mwanga kwani nikajua wale watu wamezunguka wananisubiria upande wa pili wa lilie shimo,sikutaka kurudi nyuma nikasogea mbele tu lakini jambo la kushukuru kumbe ule mwanga niliouona ulikuwa ni mwanga wa jua,nikasogea mpaka kwenya mlango lile shimo nikaangalia pande zote lakini sikuona mtu wala kitu cha hatari,nikatoka kwenye lile shimo mida ya saa moja asubuhi.
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………….
Baada ya maisha yenye visa kama vile niliacha kusikiliza mambo ya waganga nikaamua kuitunza familia yangu nikiwa pamoja na wake zangu wote hadi watoto wangu wale wawili wa kike wakabahatika kuolewa na nikapata kiasi kikubwa cha ng`ombe jambo ambalo lilinifurahisha sana,mwanangu wa kiume masumbuko muda wale dada zake wanaolewa yeye ndiyo kwanza matokeo ya kuhitimu darasa la saba yalikuwa yametoka na alichaguliwa kwenda kwenye shule ya sekondari ya kata inayoitwa sapiwi secondary mkoani simiyu,muda ulipofika wa kwenda shule niauza ng`ombe watatu waliotokana na mahari za binti zangu wawili baada ya hapo masumbuko alianza shule,masumbuko alikuwa na uwezo mkubwa sana darasani na kila siku za mwishoni mwa juma(weekend) alikuwa anarudi nyumbani kutusaidia kazi za shamba na kuchunga pia.
Ilikuwa ni siku moja ya jumapili,kama kawaida yake masumbuko alikuwepo nyumbani kutusaidia kazi siku hiyo alienda kuchunga na aliporudi hata kabla ya kula chakula cha usiku alinifuata nilipokuwa nimekaa nikiwa naota moto pembezoni mwa zizi,masumbuko alionekana anamawazo mengi sana na ilionyesha alikuwa na jambo lakunambia baada ya kusisimama kwa muda alichukua gogo lilokuwepo jirani akakaa akaanza kuota moto pia.

Vipi mwanangu nambie tu unasumbuliwa na nini? nambie

Kusema ukweli baba mimi sielewi hata nianzie wapi,nilipokuwa natoka kuchunga nikiwa nakaribia kwenye shamba letu la mahindi nilisika sauti za wanawake wawili zinaniita hata nilipogeuka sikuona mtu,baada ya kutoona mtu nikaamua kwendelea kuja nyumbani lakini baada ya hatua kama 10 nilihisi kuna mtu alinishika mikono yangu hadi nikashindwa kutembea ila ghafula nikasukumwa nikaanguka hadi nikachubuka hapa mkononi

Pole mwanangu,tambua ukimwona nyani mzee jua kakutana na mishale mingi,na sasa ndiyo unakua mwanangu yote hayo yataisha usiwe na hofu,sawa?

Sawa baba

Niliamua kumtoa hofu masumbuko lakini hofu kubwa nilikuwa nayo mimi sikutaka tena nianze kushuhudia matukio ya kichawi maishani mwangu,tuliendelea kuota moto mimi na mwanangu masumbuko hadi chakula kilipoletwa tukala pamoja ugali na maziwa na ulipofika muda wa kwenda kulala tukaagana ila mimi hofu ilizidi kunitawala juu ya tukio la mwanangu kuitwa na sauti za watu wasioonekana.
Nilijilaza kitandani lakini usingizi haukupatikana maana mawazo niliyokuwa nayo ni juu ya alichonieleza masumbuko mambo yaleyale yaliyonitesa mimi kwenye maisha yangu niliwaza kwanini muda ule yalitaka kuanza kumsumbua mwanangu,kwa muda wote usiku ulikuwa tulivu hadi ilipofika saa sita kuelekea saa saba  kutokana na saa ya kwenye simu yangu ya nokia tochi niliyokuwa nayo,kwa mbali sauti ya fisi ilisikika na kuwafanya mbwa wangu wabweke kwa sauti kali kama kawaida ya kijijini mbwa wakibweka lazima kutoka nje ya nyumba ili kuangalia kipi kinawasumbua mbwa maana unaweza kuendelea kulala ukakuta ng`ombe wote wameibiwa au wameuliwa na fisi,nilijifunga rubega kitenge cha mke wangu mkubwa maana siku ile nililala kwake nikachukua upinde na mishale yakutosha na tochi ambayo ilikuwa na betri mpya kabisa nikatoka nje,nilipokuwa pale nje naangalia usalama masumbuko naye alitoka akiwa na tochi yake yenye mwanga mkali kuzidi tochi yangu na kwa upande wake alikuwa na panga mkononi,mbwa walizidi kubweka wakiwa wanabweka kuelekea kwenye shamba lenye  mahindi jirani na zizi la ng`ombe,moja kwa moja nikajua atakuwa fisi mwenye njaa anatafuta namna ya kuingia kwenye zizi la ng`ombe,nikaichomooa mishale miwili yenye sumu nikaiwekka sawa kwenye upinde kwa ujasilili mkubwa mimi na mwanangu masumbuko tukaziwasha tochi zetu na kuelekea kule mbwa walipoelekea,tuliingia kwenye yale mahindi kwa umakini  tukawakuta mbwa wamesimama mbali ya kichaka huku wakiwa wanabweka na macho yao yote yalikuwa kwenye kile kichaka,huku tukitafakari ni kitu gani kitakuwepo kwenye kichaka na namna gani tutashambulia pale tukiwa tunaendelea kupiga hatua kusogea sauti ya mwanamke ikasikika kutoka kwenye kile kichaka na kwa haraka alisimama mwanamke akiwa mtupu kabisa kama alivyozaliwa na kwa macho yangu nikamuona mke wangu mkubwa ambaye ni mama yake masumbuko ambaye muda natoka ndani alikuwa anakoroma kabisa ila masumbuko aliposhuhudia tukio lle alizima tochi kwa  haraka…….………………………..INAENDELEA
                                                                     

Comments

Popular posts from this blog

HADITHI YA BABA MASUMBUKO SEHEMU YA KWANZA (1)

HADITHI YA BABA MASUMBUKO SEHEMU YA NNE(4)

HADITHI YA BABA MASUMBUKO SEHEMU YA TATU(3)