HADITHI YA BABA MASUMBUKO SEHEMU YA NANE(8)
HADITHI YA
BABA MASUMBUKO
Mwandishi:PAUL M,YAHILIMA
Facebook: Yahilima PM
SEHEMU
YA 8
Baada ya Yule mzee kuamuru
nikamatwe,watu wawili wenye miili mikubwa walisimama kutokea nyuma ya lile
kundi la wachawi wale jamaa wakaanza kuja kwa kasi sehemu nilipokuwa maana
nilikuwa bado niko mbele ya ule ukumbi nilizidi kutetemeka kadiri walipokuwa
wananikaribia nilipokuwa nimekaa sikuwa hata na nguvu ya kukimbia nikabaki
palepale,walipofika nilipokuwa wakaninyanyua kwa nguvu na kuanza kuniburuta
chini huku kila mmoja akiwa ameshika mkono mmoja mmoja,wakaendelea
kunivuta kama mzigo hadi kwa Yule mzee
aliyekuwa anaonekana kuwa mkuu wao kisha wakaniachia nikakaa chini mbele ya Yule mzee,muda wote nilikuwa natetemeka
sana na jasho jingi lilikuwa linanitoka huku mapigo ya moyo niliyasikia
yakipiga kwa kwa kasi isiyo ya kawaida,Yule mzee aliniangalia kwa makini kisha
akaamka alipokuwa amekaa kisha akanisogelea na kuanza kunikagua sehemu za mwili
wangu
Pimbi kasoro mkia wewe,umekiuka
masharti
Nisamehe,sikujua
Ndugu wageni na wenyeji huyu kijana
hapa amefanya kosa kubwa,nimemchunguza nimeona makubwa,kawaida yetu tukiwa
tunakula huwa hatuli chakula kwa vijiko kama watu wajinga wa mitaani wala
hatuli kwa viganja vyetu,kama mnavyojua sisi huwa tunakula kwa kutumia viganja
vya watu vilivyokaushwa kwa moto wa mianzi ila yeye amekula kwa kutumia viganja vyake
ambavyo ni anasa kwa gamboshi na kwingine,na ni nani kamleta huyu humu hata
kabla ya hii sherehe kuisha aondoke na aliyemwagiza kuja huku ndiye ataubeba
msalaba wa huyu pimbi wake na mtoeni haraka asiendelee kututia anasa humu
Nisamehe,sitarudia
Baada ya maamuzi ya Yule mzee wale
jamaa wawili wenye miili mikubwa walikuja tena wakaniangalia kwa muda kisha
wakaniamuru niwafuate na mimi sikuwa na ubishi,wale jamaa walitembea huku mimi
nikiwa nyuma yao hadi kwenye mlango mmoja,wakafumba macho nakuanza kuongea
maneno nisiyoyajua baada ya muda mfupi ule mlango ukafunguka tukaingia wote mle
ndani,kile chumba kilikuwa na giza sana na hewa ya mule ilikuwa nzito sana na
mimi nilizidi kuwafuata wale watu,tulitembea hadi kwenye chumba kingine kile
chumba kikafunguka chenyewe sote watatu tukaingia mle ndani tukamkuta jamaa
mmoja mweusi sana,nikiwa bado natafakari jamaa tuliyemkuta kwenye kile chumba
akaja akaniangalia kwa muda kisha akaanza kuongea na wale jamaa wawili
nilioingia nao mle chumbani sikujua walichokuwa wanaongea kutokana na kutoijua
lugha waliyokuwa wanaongea,baada ya mazungumzo ya muda mfupi Yule jamaa mweusi
tuliyemkuta mle akapiga mruzi na baada ya sekunde chache nilimwona fisi niliyeenda
naye usiku ule akiwa anakuja nilipo,alikuja hadi niliposimama,kisha wale jamaa
wakaniamba niondoke haraka eneo lile na mimi sikuchelewa nikapanda mgongoni mwa
Yule fisi nikafanya kila nilichoelekezwa na mganga wangu kuhusu namna ya
kumwendesha yule fisi,hazikupita hata sekunde kumi nikaondoka na fisi Yule kwa
kasi sana na ndani ya dakika kama 20 kwa
mbali nikaiona nyumba ya mganga aliyeniagiza,nilifika nyumbani kwa mganga hata
kabla sijashuka kwenye fisi nikamwona mganga nje ya nyumba yake
Umefanya nini sasa,yaani umeniingiza
kwenye matatizo
Lakini sikujua mashariti ya kule
Ujinga wako tu,na najutia kukuagiza
wewe na kuanzia leo tusijuane
Mganga aliongea kwa hasira hata
nilipokuwa namwomba msamaha hakunisikiliza kabisa na aliendelea kunitukana,Baada
ya majibizano ya muda mrefu na mganga aliamua kunipa masharti mapya kabisa ili
niweze kusafisha nyota yangu na nikiyakamilisha yale masharti atanipa dawa ya
kuwa tajiri sikuwa na lakujitetea
nikasubiri ni masharti gani atanipa,ilipofika mida ya saa nane usiku mganga
alitaka nimfuate na mimi nilimfuata hadi tukafika njia panda iliyokuwa jirani kabisa
na bwawa kubwa la kijiji,baada ya muda mfupi tukiwa pale njia panda,mganga
akaanza kuongea maneno yasiyojulikana huku akilia na kila mara jina langu
alilisema likifatiwa na jina la gamboshi moyoni mwangu nikajawa na uoga
nikajiuliza labda anataka kunirudisha
gamboshi tena nikaanza kufikilia kipi cha kufanya lakini nikiwa bado
nafikilia mganga alikuja nilipokuwa akanishika kichwa kwa mkono wa kushoto
kisha akanipiga kwa kitambaa cheusi alichokuwa nacho kwenye mkono wa kulia
akiwa anaendelea kunipigapiga kwa kile kitambaa taratibu nguvu zilianza
kuniishia na macho nayo yakaanza kujawa
na usingizi hata sikujua ni wapi usingizi huo ulitokea ila badaye nilipofumbua
macho nilijikuta nikiwa sehemu ambayo sikuitambua kwa mara moja na wakati huo sikuona
hata mtu mmoja na sikuona chakunisaidia huku hofu ikiwa inazidi kunipata ,hofu iliyosindikizwa
na baridi kali sikutaka kuwa mzembe nikaamua kusimama,taratibu nikavuta pumzi
ndefu kisha nikasimama ndipo nilipojua kuwa nilikuwa kwenye mlima uliopo karibu
na kijiji chetu na huo mlima unaogopesha sana hasa mida ya usiku maana wachawi
huwa wanakutana kwenye huo mlima na mara kwa mara moto huonekana kwenye ule
mlima mida ya usiku,nikiwa naendelea kufikilia nifanyeje nikahisi kama kuna mtu
ananipuliza kwenye sikio la kulia nikageuka lakini sikouna chochote,sikutaka
kupoteza muda nikaamua nishuke kwenye mlima lakini kila nilipokuwa najaribu
kutembea nilijikuta niko palepale nikajaribu kukimbia lakini nikawa palepale
hata nilipojaribu kukaa sikuweza tena nikahisi kama kuna watu wananishikilia
ili nisikae,baada ya dakika kama 30 nilisikia vishindo vya watu vinanizunguka
kisha ukimya ukatawala sikujua kipi chakufanya ikanibidi niwe mpole tu
Ahahahahahaha nimempata vipi
mmemwona?
Tumemwonaaaaaaa
Je,anatufaa au hatufai?
Anatufaaaaa!
Sauti za watu zikasikika karibu na
nilipokuwa nimesimama na baada tu ya zile sauti mwanga uliwashwa kutoka kwenye
mwenge waliobeba wale watu,hawakuwa watu wa kawaida walikuwa ni wafupi sana
akili ikanituma kuwa wale ndo ambao huitwa vibwengo na hata baada ya kuwepo kwa
mwanga pale ukimya uliendelea kuwepo wakati huo wale watu wafupi walikuwa
wamenizunguka ,mawazo yalinijaa nikiwa nawaza nifanyeje nilishitukia kofi zito likitua
kwenye shavu langu la kulia na nilipogeuka nikamkuta mganga kisha akacheka
kicheko kikubwa ambacho kiliniudhi sana nikamtemea mate mganga lakini
hakuonesha chuki yoyote akacheka tena kisha akawaamuru wale watu wake waondoke,sikujua
waliondokaje pale maana ndani ya sekunde kama tano walikuwa hawaonekani tena na
walipoondoka tu ukimya ukatanda na giza kubwa liliufunika mlima ule,mganga
akajikoholesha kidogo kisha akaliita jina langu kutokana na hasira sikuitika na
baada ya kuona kuwa simwitikii na nina hasira akanisogelea akanishika mkono
wangu wa kulia kisha akaanza kuongea maneno yake nisiyoyajua na baada ya kumaliza kuongea maneno yake ya ajabu kila
alichoniamuru nifanye sikutii ila
hakukata tamaa akaanza kunipa masharti ili niweze kusamehewa na niweze
kusafisha nyota,sharti lake la kwanza
alitaka nimtoe kafara mtu ninayempenda ili nyota yangu iwe safi na nikishatoa
kafara nitakuwa tajiri,bila kupoteza muda nilimchagua mtoto wangu wa kwanza wa
kike kutoka kwa mke wangu mdogo lakini baada ya kumweleza hilo alinitukana
sikujua kwanini kisha akadai nimchague mwingine na mimi nikamchagua Yule mtoto wa kike wa pili wa mke wangu mdogo
ila aliachia msonyo mkubwa kisha akanitukana sana akadai kuwa mizimu haipendi
kafara ya watoto wa kike ila inapenda watoto wa kiume sana hivyo akaniambia
nimtoe mtoto wangu wa kiume ambaye ni wa pekee tuliyempa jina la masumbuko
mwanangu ambaye sikuwahi kulifikilia kuja kumfanyia unyama licha ya ahadi za
utajiri na kusafisha nyota nilikataa katakata kumtoa kafara mwanangu huku
machozi yakiwa yananitoka,Baada ya maamuzi yangu mganga alienda pembeni akakaa
akaanza kuongea na watu ambao sikuwaona ila nilizisikia sauti tu muda huo roho
ya ujasili ikaniingia na nikaanza kupiga hatua ili nitoroke ila nilipoanza tu kutoroka kwenye ule mlima hata kabla sijafika mbali
walau nikaribie nusu ya mlima niweze kushuka chini nilisikia sauti ya mganga
ikiamuru nikamatwe na nikisumbua waniue nikajiuliza kipi chakufanya na
nikakiona kifo kinanikaribia....................INAENDELEA
Comments
Post a Comment